TOP NEWS

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas mattis nisi felis, vel ullamcorper dolor. Integer iaculis nisi id nisl porta vestibulum.

Sunday 26 January 2014

Mwanadada Flaviana na harakati za kutatua kero ya elimu nchini, asaidiwa na PSPF




JINA la Flaviana Matata sio jina geni masikioni mwa watu hapa nchini hususan kwa wadau wa masuala ya ubunifu wa mavazi na mitindo kwa ujumla.

Flaviana alianza jitihada za kujitangaza katika medani ya mitindo mwanzoni mwa miaka ya 2000 hasa pale alipoukwaa ulimbwende wa Miss Universe.


Flaviana ni mwanadada mrefu, mwembamba, mcheshi na mzuri kwa ujumla wake anaonekana kuwa ni mwenye malengo katika fani yake ya uanamitindo hasa pale anapounganisha mitindo na kusaidia masuala ya elimu.


Anaamini kuwa uanamitindo sio lazima tu kuonekana jukwaani au katika vyombo vya habari na katika matangazo ya biashara peke yake.


Akizungumza na gazeti hili Flaviana anasema kuwa kwake uanamitindo ni kuchukua mwonekano mzuri anaokuwa akionekana kwenye majukwaa ya mitindo na kisha kuweka katika hali halisi.


Akiifafanua zaidi hoja hiyo anasema kuwa akiwa kama mwanamitindo ambae anawakilisha vema nchi nje ya mipaka, anaona kwa inatakiwa kujichukulia kama kioo katika jamii na kuanza jitihada za kuhamaisha mabadiliko kwenye jami.


Akiwa anaamini kuwa elimu nduo chanzo cha mabadiliko katika jamii anaichukulia umuhimu mkubwa elimu hiyo kwa kuanza kusaidia wanafunzi wenye uhitaji maalum.


Anaongeza kuwa kwa kutambua umuhimu wa sekta ya elimu kwa wanafunzi ameamua kuanzisha mradi wa utoaji wa vifaa vya elimu kwa wanafunzi hasa wale waliopo katika mazingira magumu.


Anasema kuwa mazingira hayo magumu kwa wanafunzi yanatofautiana kwa kuwa wapo ambao wanakosa faraja ya moyo huku wengine wakiwa wanakosa hata vifaa vya kujisomea wakiwa darasani.


Anaongeza kuwa chini ya mradi huo wanafunzi wanapatiwa madaftari, kalamu, mkebe, mabegi na misaada mingineo muhimu ya kimasomo.


"Mimi nimechagua elimu kama ndio njia mojawapo ya kuleta chachu ya mabadiliko katika jamii, na kwa kutambua hilo ninawasaidia wanafunzi walio katika elimu ya msingi na hadi sasa ni mengi nimeshayaanza kuyafanya"alisema Flaviana.


Katika kuonesha dhamira yake ya dhati katika kusaidia watoto wenye uhitaji huo maalum wa misaada ya shule mwanamitindi Flaviana anasema kuwa tayari kwa msimuu huu wa Januari ambapo wanafunzi wanarejea darasani amewasaidia wanafunzi 1000 vifaa hivyo vya shule.


Anasema kuwa misaada hiyo imetolewa kwenye shule ya msingi Chanzige iliyopo wilayani Kisarawe ambapo wamesaidiwa wanafunzi 280 pia wanafunzi 420 wa shule ya msingi Kimanzichana iliyopo Mkuranga.


Anaongeza kuwa wanafunzi wengine ni wa shule ya msingi Msinune iliyopo Bagamoyo ambapo wanafunzi 300 wamesaidiwa.


"Sasa unaweza kuona ni kwa jinsi gani ambavyo kuna wanafunzi wamesaidiwa kupitia mradi huu ambapo wanapewa vifaa hivyo kwa bure kabisa kila mmoja na tuanzidi kujipanga kuhakikisha kuwa mwezi Julai tunasaidia wengine wengi zaidi"anasema Flaviana.


Pia mwanadada huyu anasomesha wasichana 15  ambao wanapata elimu ya sekondari katika shule mbalimbali za serikali hapa nchini.


Katika kufanikisha adhma yake hiyo Flaviana amekuwa akisaidiwa na watu mbalimbali, mfano mzuri ni Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma(PSPF) pamoja na mdau wa masuala mitindo wa nchini Marekani Russell Simons.


Flaviana anaonekana kuwa na moyo wa kushirikiana na wadau wengine katika kufanya kazi hiyo ya kusaidia watoto wenye uhitaji maalum.


Akishirikiana na Russell Simons amepewa madaftari ya mazoezi na kalamu za wino kwa wanafunzi 500 walio chini ya mradi wa Tanzania Mitindo House, The Olevolos Project ya Arusha pamoja na shule ya msingi Mwasele mkoani Shinyanga.


Kwa msaada huo wa Russell Simons katika kila mwanafunzi kwenye wanafunzi hao 500 kila mmoja atapatiwa madaftari 10 na kalamu ya wino moja.


Kwa upande wake Ofisa Uhusiano wa PSPF, Hawa Kikeke anasema kuwa mfuko huo unatambu ajitihada zinazofanywa na wasanii katika kuleta mabadiliko kwenye jamii.



Anasema kuwa kazi ya uanamitindo aifanyao Flaviana ni moja kati ya walengwa wa mfuko huo ambao uanatambua pia wafanyakazi wasiokuwa kwenye mfumo rasmi wa ajira.


Anaongeza kuwa kwa kutambua jitihada zake za kuleta mabadiliko katika jamii PSPF imeamua kumuunga mkono katika kufanikisha msaada wake wa wanafunzi wa awamu ya kwanza ya mwezi Januari wa kutoa misaada kwa wanafunzi 1000.


"PSPF inatambua nafasi za wafanyakazi kama hawa katika suala zima la kusukuma mabadiliko kwenye jamii na ndio maana na sisi tumeona kuwa ni wakati pia wa kuungana nae"Anasema Hawa.


"Wasanii, wanamitindo na hata wajasiriliamali wadogowadogo hawa wanahitajika katika mfuko huu wa PSPF sasa ni kwa nini na sisi tusimuunge mkono mwanadada kama huyu ambae ni mwanamitindo na anasaidia jamii"anasema Hawa.


Flaviana anawataka watu mbalimbali kujitokeza na kumuunga mkono katika harakati hizo ambazo amesema kuwa ni kwa faida ya watanzani kwa ujumla.
zaidi msomeni Flaviana katika www.habari5.blogspot.com
01:14 Posted by elimuboratanzania 0

Saturday 21 December 2013

Jokate anatufundisha mengi wanawake























JINA la Jokate Mwegilo sio jina geni masikioni mwa watu wengi hasa wadau wa burudani, Mitindo na hata filamu.
Mwanadada huyu amekuwa akijihusisha na masuala mengi katika jamii na amekuwa akisisika hasa kwa mtazamo chanya.
Amekuwa akitumia muda mwingi katika kufanya mambo ambayo yanang'arisha nyota yake huku akitumia muda wake mwingi katika kufanya kazi.
Hivi majuzi alizindua huduma mpya ya kutoa ushauri katika masuala ya urembo kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kwa njia ya simu.
Kurasa wa Nyota Jumapili ulifanya jitihada za kutaka kufahamu mengi kuhusiana na mwanadada huyo na kile kilichomsukuma hadi kuanzisha huduma hiyo.
Akizungumzia uamuzi wake wa kuanzisha huduma hiyo ambayo mteja anatakiwa kutuma neno Kidoti kwenda 15678 ,  anasema kuwa kuanzia mwaka jana alianzisha huduma ya nywele ya Kidoti ambayo ilikuwa na lengo la kuwarembesha wanadada.
Anasema kuwa yangia hapo aliendelea na biashara hiyo ambayo alisema kuwa imekuwa ikiendelea vema kwa kiasi kikubwa.
Anaongeza kuwa baada ya kuendelea na biashara hiyo kwa muda mrefu kukawa na changamoto kubwa kutoka kwa wanadada ambao walikuwa wakitaka kuelimishwa masuala ya urembo na hapo ndipo akaamua kuwafikia kwa kutoa huduma hiyo ya ushauri wa urembo wa njia ya meseji.
"Najua mimi mbali na kuwa mbunifu katika kufanya biashara zangu za kukuza maisha lakini pia najaribu kufanya kila niwezalo kuwafikia wadada wenzangu na kujadiliana na nao masuala mbalimbali kama hivi urembo"anasema Jokate.
Anaongeza kuwa kwake anatambua kuwa kila mwanamke anaweza kuwa mrembo kwa kuwa urembo unaweza kutengenezwa lakini kwa upande wa uzuri hicho ni kitu cha kuzaliwa nacho.

Lakini hata hivyo anaongeza kuwa urembo peke yake sio kila kitu kwa mwanamke ambapo anawaasa wanawake wenzake kujituma na kutumia ubunifu zaidi katika kusaka maendeleo pia.
Anaongeza kuwa maendeleo kwa mwanamke ndio yatamwezesha kujipatia mahitaji mengine yote muhimu ukiwamo urembo pia.
Anatolea mfano nafsi yake kwa kuanzisha biashara ya nywele za Kidoti ambazo zinauzwa sana katika maduka ya Kariakoo na pia mikoani zimekuwa zikichangamkiwa zaidi.
Katika kuthibitisha dhana nzima ya kutafuta maendeleo ya kimaisha Jokate amejiingiza kwenye filamu za Bongo Movies.
Kwa sasa ameshakamilisha filamu moja kaiwa na mwigizaji Jacob Steven, JB ambayo inaitwa Mke Salama ambayo mwakani inaingia sokoni.
Anasema kuwa filamu hiyo imegusia masuala mbalimbali ya kimaisha likiwamo suala ya mapenzi na mengineo.

Lakini pia ameimba wimbo mmoja na msanii Luci uitwao Kaka na Dada ambao unaendelea kutamba kwa sasa huku akiwa anamhusudu zaidi msanii Judith Wambura, Lady Jaydee, Ay na Mwana FA.
Akizungumzia mikakati yake zaidi kwenye filamu anasema kuwa anataka mwakani kutoa albamu yake ambayo inaendelea kupikwa kwa sasa.
Anasema kuwa anataka kuendelea kufanya vema katika muziki hasa kutokana na kuwa na kipaji cha kuimba kucheza muziki.
Anasema kuwa kwa sasa bado hajaanza kupokea shoo za muziki na anaongeza kuwa pindi akimaliza nyimbo zake ataanza kupokea shoo ndani na nje ya nchi.
Jokate ambae ni mrefu wa wastani, mweupe, mchangamfu anaonekana kuwa ni mdada mwenye mambo mangi kichwani mwake.
Kujihusisha kwa mambo mengi kwa muda mfupi imewafanya watu wahisi pengine hajitambui na hajui nini anachotaka kukifanya.
Akizungumzia hilo anasema kuwa anajua kila kile anachoamua kukifanya na anataka kutumia muda wake mwingi kama mwanadada kijana kujtuma zaidi kwa kipindi hiki katika kutafuta hela.
"Najua mimi sio mwanamke wa kutegemea kupewa mbali na kuwa mzuri nina jina kubwa lakini sipendi kabisa masuala ya kutegemea wanaume kunipatia hela au kunitunza hiyo mwiko kwangu"anasema Jokate.
Akilifafanua hilo la kutotegemea mwanaume kumsaidia katika kujitafutia maendeleo anafafanua kuwa kwa wadada wengi hasa wenye majina wanategemea kuwekwa mjini na wanaume zaidi.
Anaongeza kuwa kwa upande wake kwanza kwa sasa hana mpenzi na hatarajii kwa sasa ila anachokifanya kwa sasa ni kuhangaikia hela.
Anaongeza kuwa anataka mwaka ujao aongeze mtaji wa biashara zake hadi kufikia zaidi ya milioni 200.
"Naamini kuwa naweza, nitaweza na lazima niweze kufikia malengo yangu tena mimi kama mimi najua mimi sitaki umaarufu wa kijinga yani kujifanya nionekane wa maana kwa fedha za kupewa"Alisema Jokate.
Maisha ya Jokate katika elimu yake ni kwamba amefanya shahada ya Political Science na aliamua kuachana kujiendeleza katika masomo zaidi.
Anasema kuwa alikuwa ameanza masomo ya Shahada ya Uzamili lakini hata hivyo alilazimika kuahirisha baada ya kutingwa na mambo mengi.
Lakini hata hivyo anafafanua kuwa kwake anapenda kufanya yale ambayo moyo wake unaridhia na kuongeza kuwa hilo limekuwa likimsaidia kufanikiwa katika mengi.
Mwanadada huyu ambae anawapenda wanasiasa kama akina John Mnyika ambae ni Mbunge wa Jimbo na Ubungo pamoja na Zitto Kabwe, anasema kuwa anaipenda na kuichukia siasa.
Anapenda kula na kuimba pamoja na kukutana na watu wapya kila siku huku akipenda zaidi kufanya shughuli za kijamii.
Anawataka wasichana wenzake kujituma na kuepuka kutumiwa kwa mambo mbalimbali ambayo yanadharirisha utu wao.
Anampenda zaidi Rais Jakaya Kikwete ambapo hakusita kuisifia hotuba yake ya hivi karibuni aliyoitoa wakati wa maziko ya Rais wa kwanza mwafika wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.
Anasema kuwa imewaelewesha watu duniani nafasi ya Tanzania katika kukuza demokrasia barani Afrika.
Jokate ni mdogo wa Constantine Magavila mmoja kati ya vijana ambao wamekuwa wakizungumzia masuala mengi kuhusiana na maendeleo ya vijana.
Pia anae dada yake aitwae Dessy Deria, na mdogo wake Martn Kalikali.
Aliwahi kushika nafasi ya pili katika shindano la Miss Tanzania mwaka 2006 ambapo mwaka huo huo Wema Sepetu ndio aliibuka na ushindi wa taji hilo.
Mwisho 
07:16 Posted by elimuboratanzania 0

Sunday 15 December 2013

Endelea kujionea yaliyojiri Swahili Fashion




































"Kwa mwaka huu ambapo nimeonesha nguo zangu kadhaa naona kuwa kwangu ilikuwa ni fursa pia ya kukutana na kujifunza kutoka kwa wenzangu"alisema Zamda.


Onesho la Swahili fashion mwaka hu lilifanyika kwa siku tatu na kuwakutanisha wabunifu zaidi ya 30 huku wengine wakiwa wametokea nchi za nje Afrika Mashariki na Afrika nzima kwa ujumla.
Mwisho
05:21 Posted by elimuboratanzania 0