TOP NEWS

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas mattis nisi felis, vel ullamcorper dolor. Integer iaculis nisi id nisl porta vestibulum.

Friday 15 February 2013

Goldie Havery mchumba wa Prezoo afariki dunia

Goldie ndo huyo alikuwa hote lady kweli kweli

MSANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya Ambwene Yesaya, AY, amesikitishwa na kifo cha msanii mahiri wa nchini Nigeria Goldie Harvey ambae pia aliwahi kushiriki katika shindano la Biog Brother Africa 2012

Goldie ambae aliwahi kuimba wimbo uitwao Skibobo akishirikiana na AY ambapo wimbo huo uliweza kuanza kutimiza ndoto za AY kuimba na wasanii wa Nigeria huku na msanii huyo ndio alikuwa ndio msanii wa kwanza kutoka nchini Nigeria kuimbana AY.

AY aliliambia gazeti hili kwa njia ya simu kuwa alikuwa akimkubali sana msanii huyo kwa kuwa alikuwa ana ushirikiano mzuri na alikuwa na mapenzi na wasanii wa Afrika Mashariki.

Alisema kuwa alimfahamu Goldie kupitia msanii Prezoo wa nchini Kenya aliyekuwa na uhusiano na Goldie, AY alisema kuwa Goldie alikuwa na ndoto kubwa na alikuwa tayari ameanza kufanya kazi nae na walikuwa na malengo makubwa mengi zaidi.

“ Yani huku alikuwa ni msanii wa karibu sana na wasanii wa Afrika Mashariki na hivyo pia ilikuwa ndio nafasi za awali za kuanza kufanya kazi na mdau huyu nap engine tungefika mbali zaidi” alisema AY.

Msanii huyo aliyejichukulia umaarufu pia katika ukanda huu wa Afrika Mashariki kutokana na uhusiano wake wa kimapenzi na msanii Prezoo wa nchini Kenya waliekutana katika shindano hilo la BBA 2012.

Goldie aliaga dunia mapema juzi ambapo kwa mujibu wa meneja wake aitwae Keke Ogungbe alisema kuwa Goldie aliumwa sana kichwa na wakampikimbiza hospitali ambapo alifariki dunia muda mfupi baada ya kuwasili hopsitalini hapo.

Golidie aliwahi kusikika akihojiwa katika  kituo kimoja cha Luninga hapa nchini akisifia ukarimu na uwezo wa wasanii wa hapa nchini na kusisitiza kuwa angependa kufanya kazi zaidi na wasanii wa hapa nchini.
Mwisho

0 comments: