Quen suzy kuingia bongo fleva
MCHEZA
muziki wa bendi ya FM Academia Queen Suzy ameamua kujikita katika muziki wa
kizazi kipya.
Akizungumza
na safu hii Queen Suzy alisema kuwa kwa sasa ameanza kurekodi wimbo wake wa
mapenzi wa muziki wa kizazi kipya.
Alisema kuwa
anaona mbali na kuwa mchezaji mahiri wa muziki wa dansi lakini anaiona fursa
kubwa katika muzii wa kizazi kipya.
" Najua
katika maisha kuna mambo mengi ya kujiendeleza mimki naona kuwa mbali na kuwa
ninamiliki baa na kujiongezea kipato lakini ngoj akidogo niguze kwenye muziki
wa kizazi kipya"alisena Suzy.
Alisema kuwa
uwezo wa kucheza muziki alionao unaweza kumsaidia kujitangaza zaidi kimuziki
kwa kuwavutia wapenzi wake wa muziki.
Alisema kuwa
amejipanga kuimba nyimbo za aina zote kuanzia muziki wa kisasa hadi miziki ya
zamani na kuongeza kuwa hiyo ni hatua kubwa kwake akiwa kama mcheza muziki na msanii wa muziki.
0 comments: