TOP NEWS

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas mattis nisi felis, vel ullamcorper dolor. Integer iaculis nisi id nisl porta vestibulum.

Monday 7 January 2013

Madada kuna aina zaidi ya 50 za embe poa kwa msosi




Hapo kuna embe Alfons, embe Apple na nyingine kibaooo

Watu wakaanza kuzionja kama kawa

hawa ni wadau wa shamba la Kilodede

Watu walinawishwa na kuonjeshwa embe hapohapo    



Mwenyekiti wa Chama Cha Wakulima wa Embe (Amagro) Burton Nsape akizungumza kuhusiana na namna ambavyo chama chake kinawasaidia wakulima wa embe kujipatia kipato kupitia zao hilo anasema kuwa Amagro hutoa elimu kwa wanachama wake.

Nsape anasema kuwa wakulima mbalimbali walikuwa wakilima na kuuza hadi nje ya nchi embe kw amuda mrefu ambapo anafafanua kuwa ni biashara nzuri na yenye faida kubwa.

Anasema kuwa Amagro inaendeleza harakati za kuwapatia wanachama wake elimu ya maarifa mbalimbal kuhusiana na ukulima wa zao hilo kama vile namna ya kudhibiti wadudu waharibifu, namna ya kufunga na kuhifadhi embe ikiwa pamoja na matumizi ya madawa na mbolea.

Anasema kuwa changamoto kubwa inayowakabili wakulima wa embe ni ukosefu wa usafirishaji wa kitaalamu kutoka mashambani hadi kuelekea kwenye soko kwa kuwa ili kuweza kuliweka embe katika ubora wake kuna mengi zaidi ya kuyafuata.

Akizungumzia kuhusiana na aina ya embe na ubora unaotakiwa katika soko la nje anasema kuwa kuna aina zaidi ya 1000 ya embe duniani kote.

Anafafanua zaidi kuwa kwa hapa nchini kwa muda mrefu tumekuwa tukilima embe za asili ambazo soko lake kwa nje sio kubwa.

Anasema kuwa katika tani laki 3.72 za embe ambazo hupatikana hapa nchini takribani kila mwaka ni asilimia 10 tu ambazo ni embe za kisasa huku nyingi zikiwa ni zile za asili.

Anasema kuwa Amagro imeamua kuwahamasisha wakulima ambao ni wanachama wake kuzalisha aina ya nne za embe ambazo ni Apple, Keit, Muyuni na Alfonso.

Anasema kuwa angalau wakiwa na aina hizo za embe wanaweza kuwa na uhakika wa kupeleka embe na kuuza nje ya nchi kwa kuwa hizo ni moja kati ya aina za embe ambazo zinatakiwa zaidi nje.

0 comments: