Ally Choki aikubali Kili Awards
MSANII wa
muziki wa dansi nchini Ally Choki amepongeza utaratibu uliotumika kuchagua
washiriki wanaowania tuzo za Kili 2013.
Choki ambae
miaka iliyopita aliwahi kusema kuwa hataki kushirikishwa kabisa katika tuzo
hizo kwa kuwa hakukubaliana na utaratibu uliokuwa ukitumika kuchagua washiriki
Akizungumza
na kituo kimoja cha Radio Choki alisema kuwa awali walikuwa wakiwaweka katika
kipengele kimoja wagombea ambao muziki wao ulikuwa hauendani.
" Kwa
mwaka huu naona kuwa angalau kile nilichokuwa nikikipinga kimefanyiwa kazi kwa
kuwa hata wagombea wamewekwa wale ambao wanaendana hasa katika kipengele cha
muziki wa dansi" alisema Choki.
Alisema kuwa
zamani aliwahi kuwekwa katika kipengele kimoja na wasanii kama vile Gurumo na
wengineo ambao ni magwiji wa muziki huo.
Alisema kuwa
kwa yeye kushindanishwa na watu kama hao ni kosa kwa kuwa wanawekwa kwenye
kundi la watu ambao wote wanaimba muziki wa dansi kwa kuwa wanaimba kwa nyakati
tofautitofauti.
Alisema kuwa
bendi kama za Msondo na Sikinde wanaimba muziki wa dansi kwa kizazi ambacho ni
tofauti na hiki cha akina Choki, Banza, Muumini na Khalid Chokoraa.
Hata hivyo
alisema kuwa yupo tayari kushiriki michuano hiyo ya Kili iwapo utaratibu
ukiendelea kuwa mzuri kama ulivyo sasa.
==============
0 comments: