Msanii Ommy Dimpoz mzee wa madada awahasa wasanii wakongwe
WASANII wa
muziki wa kizazi kipya ambao wamekuwa wakiimba kwa muda mrefu wametakiwa
kutokata tamaa ya kazi zao hata kama wamesota muda mrefu bila ya mafanikio.
Hayo
yalisemwa na msanii Omary Nyembo, Ommy Dimpoz, ambapo alisema kuwa
anasikitishwa na wasanii kama hao ambao kwa sasa wanashinda wakilalama tu kuwa
hawana bahati.
Alisema kuwa
wasanii kama hao wanakuwa hawajisikii vema kuona kuwa kuna wasanii wapya
wanakuja katika fani ya muziki na kuwakuta na kisha kuwaacha.
Alisema kuwa
kawaida muziki una wakati na iwapo msanii wakati wake ukifika ndio anatakiwa
kuutumia vema kujiimarisha katika soko.
" Mimi
nashangaa sana utakuta mtu msnaii lakini
katika mazungumzo yake anakuwa haishi kulalama kuwa mara hoo wao hawatoka na
mengine mengi inachotakiwa ni kujipanga sio lawana" alisema Ommy Dimpoz.
Kwa sasa
Ommy Dimpoz ni mmoja kati ya wasanii wachache waliopo kwenye chati ya muziki wa
kizazi kipya hapa nchini.
Msanii huyo
amechaguliwa kugombea tuzo sita katika mashindano ya Kili Music kwa mwaka huu
ambapo ameongoza kuwa msanii aliyechaguliwa katika tuzo nyingi.
0 comments: