Sina Bifu na dingi wangu-- Q chief
MSANII wa
muziki wa kizazi kipya Q Chilla amekanusha kuendelea kwa ugomvi dhidi ya baba yake mzazi.
Q Chief
alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati akifanya onesho lake katika klabu ya
maisha.
Alisema kwa
awalia alikuwa katika mzozo na mzazi wake huyo lakini kwa sasa hana tatizo nae
tena.
" Kama
mnakumbuka hata zile nyimbo zangu za mwanzo nilikuwa ninaziimbaje yani nilikuwa
ni kama vile kuna vijembe fulani lakini kwa sasa mambo yangu na mzazi wangu
huyu ni mazuri sana tu"alisema Q Chief.
Naye mzazi
huyo akizungumzia muziki wa Q Chief alimtaka aimbe na kufika kiwango cha
kimataifa.
Alisema kuwa
anaipenda kazi ya mtoto wake huyo na imemsaidia kufikia malengo yake mbalimbali
na hakusita kumwagia baraka zake Q Chief.
" Mimi
kama mzazi namtakia maisha mema kijana wangu huyu ili afike katika ngazi za
kimataifa kwa kuwa uwezo anao na kila sababu ya kufanya hivyo ipo"alisema
mzazi wa Chief.
0 comments: