MBUNIFU wa
mavazi mahiri nchini anayetamba na lebo yake ya Eskardo Bird aitwae Doreen Noni kwa sasa awasisitizia
wasanii kuwa na wabunifu wao wa mavazi pia.
Doreen ambae
pia ni mtaalamu wa masuala ya upangiliaji wa mavazi amehusika kwenye kuwapangia
mavazi wasanii wanaoshiriki kwenye mchezo wa kuigiza wa Siri ya Mtungi.
Doreen pia
alihusika kwenye kuwavalisha washiriki wa shindano la Epi Bongo Star Search kwa
mwaka 2012.
Mwanadada
huyo alisema kuwa wasanii mbali na kuwa ni kioo cha jamii lakini pia wanatakiwa
kujitambua kuwa mavazi yanaweza kuwaongezea umahiri katika kazi zao.
Alisema kuwa
iwapo wasanii wakitambua nafasi ya mavazi katika kuimarisha haiba yao kisanii
hawatasita kuwatumia wataalamu wa mavazi katika kuwapangia kuvaa.
" Naona
kuwa wasanii wa hapa nyumbani wakijipanga na kutumia ghara ma kidogo katika
kupanga mavazi basi watakuwa wamefanya kitu muhimu kwa kuwa nafasi ya mavazi ni
kubwa katika kazi za sanaa hapa nchini" alisema Doreen.
|
0 comments: