TOP NEWS

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas mattis nisi felis, vel ullamcorper dolor. Integer iaculis nisi id nisl porta vestibulum.

Monday 13 May 2013

Ni muhimu kuisoma hii


Na Evance Ng'ingo
KAMA ikiulizwa moja kati ya taarifa za habari za burudani na sanaa ambazo zilitawala katik avyombo vya habari mbalimbali hapa nchini kwa siku kadhaaa zilizopita basi ni mzozo kati ya msanii wa muziki za kizazi kipya Judith Wambura na Kituo cha Clouds FM.

Sakata hilo lililodumu kwa muda wa siku kadhaa ambapo upande mmoja ulikuwa ukishambulia zaidi na hadi upande wa pili wa Clouds Media ulipoamua kulitolea ufafanuzi suala hilo.

Yapo mengi ya kujifunza na ambayo wasanii kwa ujumla wanatakiwa kujifunza katika kipindi hiki cha siku hizo ambazo yalikuwapo hayo malumbano.

Zipo hoja nyingi ambazo zilitolewa na Lady Jaydee ambapo moja kati ya hoja kubwa aliyokuwa akiilalamikia ni kuhujumiwa kwa nyimbo zake kutochezwa katika kituo hicho cha Radio.

Hiyo ilikuwa ni ndio hoja kubwa zaidi ambayo ilipelekea kwa msanii huyo kujikuta akisisitiza kuwa hata akifariki dunia baso viongozi wa kituo hicho ambayo ni Joseph Kusaga ambae ni Mkurugenzi Mtendaji pamoja na Rugemalila Mutahaba ambae ni Mkurugenzi wa utafiti wasifike kwenye maziko yake.

Binafsi naona kuwa kwa hoja kama hiyo na nyinginezo zinanipatia picha kuwa wasanii wengi wamekuwa na mtazamo wa kufikiria zaidi nyimbo zao kufahamika kupitia radio zaidi.

Nikisema kuwa wasanii wanatakiwa kuw ana mengi ya kujifunza ni hasa katika kuangalia njia mbadala za kuhajkikisha kuwa nyimbo zao zinasikika hata bila ya kuwepo kwa radio.

Nampongeza Jide kwa kuhakikisha kuwa ameamua kuuza albamu yake kwa njia za kisasa kabisa ambapo anawatumia wauzaji wa mtandao wa Max Malipo ambapo albamu yake nzima itakuwa ikiuzwa.

Umakini kama huo katika ubunifu ni umakini ambao unatakiwa kutumika katika kuzitangaza nyimbo zake pamoja na kuhimili ushindani wa aina mbalimbali.

Kwa msanii mkubwa kama yeye sio kitu cha kuwafurahisha wapenzi wake wa burudani kusikia kuwa analalamikia nyimbo zake kutochezwa na kituo kimoja cha radio.

Ikifika wakati msanii akajiingiza katika malumbano kama hayo ni dhahiri kuwa hata wapenzi wake wa muziki nao wanakuwa ni kama wapo njia panda kwa kuwa sio wanachotakiwa kukisikia kwa muda huu wa matayarisho ya uzinduzi wa albamu.

Suala la nyimbo za wasanii kutochezwa kwenye vituo vya radio sio geni kwa kuwa wasanaii wengi ambao nao pia walijikuta nyimbo zao hazichezwi radioni kwa sababu mbalimbali.

TID ni mmoja kati ya wasanii ambao nyimbo zao ziliwahi kupigwa marufuku kuchezwa kwenye kituo cha Clouds na lakini hata hivyo aliweza kumaliza sakataka hilo.

Msanii Rehema Chalamila, Ray C nyimbo zake ziliwahi kuzuiliwa kuchezwa kwenye kituo cha East Africa Radio hadi alipoomba msamaha na hata kwa sasa Diamond nae amekuwa kwenye sakata kama hilo pia kwa radio ya Magic Fm.
Hivyo kukataliwa msanii kuchezwa nyimbo zake sio geni kwa sekta hiyo ya sanaa hapa nchini lakini hata hivyo suala linabakia kuwa ni haki kutochezwa nyimbo zao redioni.

Rugemalila Mutahaba analizungumzia suala hilo kuwa hata msanii mahiri wa muziki wa Marekani  Kanye West alipokosea katika tuzo za MTV kituo hicho cha Luninga kilikataa kucheza nyimbo zake kwa muda.

" Ikumbukwe kuwa hivi ni vituo binafsi vya Radio na iwapo mtu akikosea basi au akifanya mambo ya utovu wa nidhamu ipo haki ya kuadhibiwa kwa namna mbalimbali, sisi kama Clouds nyimbo za Jide tumezicheza mara nyingi sana tu lakini amekuwa akitukejeli katika mitandao ya kijamii na kwengineo" anasema Ruge.

Anafafanua kuwa "kituo hiki kimeamua kuacha kutumia nyimbo za msanii huyo kwa kuwa hata mwenyewe alisema kuwa ana mpango wa kufungau kituo chake cha radio na alisema kuwa hana haja ya nyimbo zake kuchezwa huku kwetu, sasa sisi tumazimishe ya nini".

Nikisema kuwa yapo mengi ya wasanii kujifunza ni moja kuhakikisha kuwa watafute wataalamu watakaowawezesha kujua namna ya kuzitangaza nyimbo zao hata kwa kutumia blogs, tovuti na kwengineko.

Hapa pia linakuja suala la umuhimu wa kuwa na wataalamu katika masuala ya Utawala wa Sanaa (Art Management), kama wakiwepo hao sio rahisi kwa msani kujikuta akiiingia katika marumbano au mtafaruku wa aina yoyote ile ya sanaa.

Huenda hata hili la Jide lisingefikia hatua kama hiyo iliyofikia ya hadi watu kutukanana katika mitandao ya kijamii.

Au huenda kuna ukweli kuwa eti Jide ameshindwa kuhimiri ushindani ambao kwa sasa unamkabili hususan ujio wa bendi ya Skylight iliyochukua wasanii wengi kutoka kwenye bendi yake ya machozi.

Kwa sasa bendi hiyo ina wateja wengi zaidi huku wakiwa na mikakati mizuri ya kutumia fursa za kujitangaza zilizopo kuanzia katika radio, blogs na magazeti.

Kwa sasa bendi hiyo ambayo haina wasanii wenye majina makubwa sana lakini ndio katika hafla mbalimbali na hata shoo zao wamekuwa wakipata watu wengi.

Iwapo hiyo ni moja kati ya sababu za mjadala wote huo nandio ukapelekea kuwatolea maneno wamiliki wa kituo hicho basi ni vema hapa ukatumika zaidi ule ueledi wa masuala ya Arts Management.

Hapa nikiwa na maana ya kuwa jaribu kujisoma na kuangalia futrsa iliyopo katika kujitanua zaidi na kuuhimili ushindani.

Jina lako ni kubwa na wewe unaweza kujipanga na kuendelea kuwa na wateja wako kama kawaida sasa kama wakati upo na waimbaji kama Sam Machoz, Mwinyi na wengineo ulikuwa unaweza panda jukwaani kuanzia saa sita au saba sasa anza mapema zaidi.

Usibakie kuwa muimbaji bali pia ingia kwenye hatua ya uburudishaji zaidi kwa kucheza na kuimba ili kuwafurahisha zaidi wateja wako.

Gadner Habash ambae ni Meneja wa Jide anasema kuwa kwa sasa msanii huyo anakuja na staili mpya ambazo pia zitaendeelea kumweka kwenye chati.

Hatua hiyo ni muhimu kwa kuwa hata kama wapo wasanii ambao waliamua kurudi na kuomba suluhu kwenye vituo vya radio walivyokorofishana navyo.

Kwa sasa wapo wadau mbalimbali ambao wanashauku ya kuendelea kuzisikia nyimbo za Jide katika radio hiyo

Mmoja kati ya wadau hao ni  naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Amos Makalla ambae amejitokeza wazi na kutaka kuwepo kwa suluhu.

Anasema kuwa yupo tayari kukutana na pande hizo mbili kusaka suluhu la kudumu la mgogoro huo, akisema malumbano hayana tija na yanakuza mgogoro.
“Kutokana na malumbano ya Jide (jina jingine la Jaydee) na uongozi wa Clouds, natoa mwito nikutane na pande mbili. Nawasihi sana malumbano hata hayatakuwa na tija, bali kukuza mgogoro uliopo sasa,” alisema Naibu Waziri Makalla.

 “Sifurahi hata kidogo jambo hili linaloendelea halijengi. Nimsihi sana mdogo wangu na shemeji yangu Jide, akubali tukae pamoja na niwaombe Clouds wakubali tukae pamoja. Naamini tukikaa pamoja tutaongea jambo hili litakwisha,” alisema Makalla.

Hata hivyo huenda hatua hiyo ya makala ikatatua mgogoro huo na kujikuta wapenzi wa Jide wakiendelea kuzikisikia nyimbo zake kituoni hapo kwa kuwa hata Ruge aliwahi kumsihi Jide atafute watu anaowaamini ili wawasikilize pande zote mbili na kutafuta muafaka.
Mwisho

0 comments: