TOP NEWS

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas mattis nisi felis, vel ullamcorper dolor. Integer iaculis nisi id nisl porta vestibulum.

Sunday, 12 May 2013

Sina mpnago kabisa na X Factor --- Gamu



MSHIRIKI wa shindano la uimbaji la X Factor Gamu Nhengu amesema kuwa hata akipata nafasi ya kuimba kwa mara ya pili katika shindano hilo hatoweza kufanya hivyo.

Gamu alitolewa katika shindano la mwaka 2010 na jaji was shindano hilo Cheryl Cole baada ya kushawishiwa na Cher Llyod.  

Gamu ambae ni raia wa nchini Zimbabwe yeye pamoja na familia yake walituhumiwa kujihuisha na masuala ya ubadhirifu na kisha wakatishiwa kurudishwa nchini mwao kutoka Uingereza.

Lakini hata hivyo baadae aliruhusiwa kuendelea kuishi nchini humo kwa sasa amekuwa akitumikia mkataba wake wa kuimba kwa miaka miwili akiwa anaandaa albamu yake ya A Love Like This. 

Alisema kuwa " hata leo hii nikitapa nafasi ya kufanya vitu vyangu katika onesho hilo sijui yani hata itakuwaje kwa kuwa sina mzuka tena" alisema Gamu.

Kwa sasa anatamba na wimbo wa A Love Like This uliobeba jina la albamu hiyo pia anatarajia kuachia wimbo mwingine.

Alionesha kuishukru studio aliyoiita kuwa ni ndoto iliyopo nchini Scotland na kuongeza kuwa imemsaidia kurekodi wimbo huo mmoja ambao anasema kuwa asingeweza kufanya hivyo iwapo angeshinda shoo ya X Factor.


0 comments: