TOP NEWS

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas mattis nisi felis, vel ullamcorper dolor. Integer iaculis nisi id nisl porta vestibulum.

Sunday, 12 May 2013

Chris Brown na Rihana, we acha tu!


LILE sakata la kuachana kwa wasanii mahiri wa muziki wa kisasa nchini Marekani Chris Brown and Rihana waliokuw ana uhusiano wa kimapenzi kwa sasa  limechukua sura mpya baada ya kudhihakina kwenye mtandao wa kijamii wa twitter.

Katika kuonesha kuwa anamtupia kijembe mpenziwe huyo ambae kwa sasa sio wake tena Rihana aliandika kwenye akaunti yake ya twitter kuwa  ana kitu kwa ajili ya watu wa zima na kusisitiza kuwa Brown sio mtu mzima.

Hoja hiyo ilionekana kuwagusa wengi ambao kwa sasa wanaonekana kuwa wamekuwa wakifuatilia ugomvi wao huo kwa muda mrefu.
Utata huo ulianzia zaidi Jumatano iliyopita ambapo Chris Brown aliandika kwenye akaunti yake ya twitter kuwa hawezi kufikiria kuwa kuoa mtu ambae bado ni mtoto.

Hapo hapo Rihana naye alijibu kuwa hana mpango wa kujiweka zaidi ya kuzingatia kuwa na heshima, upendo na hadhi  kwa asilimia 100 na mapenzi sio kwa ajili ya watoto.

Wasanii hao walihi kuwa na uhusiano wa kimapenzi kabla ya kutengana ambapo Chris Brown aliwahi kuamriwa na mahakam kuwa asimsogelee msichana huyo kutokana na kitendo cha kimpiga.

Hivi karibuni walirudiana tena na kuwa katika uhusiano ambapo haukudumu kama ule wa awali na kwa sasa wametengana tena.


Rihana alionekana mitaa ya New York akidhurura na ambapo inasemekana kuwa amerejesha uhusiano wake na JR Smith aliyekuwa mpenzi wake na akijibu hilo Chris Brown alisema kuwa Rihana kuwa sio wake ila ni wa mtu mwingine kwa sasa.


Hata hivyo kijana huyo alimwalika mpenziwe wa zamani Karrueche Tran kwenye sherehe yake ya kuzaliwa muda mfupi kabla ya kuzungumzia kuvunjika kwa uhusiano wake na Rihana.


0 comments: