TOP NEWS

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas mattis nisi felis, vel ullamcorper dolor. Integer iaculis nisi id nisl porta vestibulum.

Sunday, 12 May 2013

Utoto wa Justin Bieber waacha gumzo Dubai





Baada ya kukumbana na kisanga cha kupigwa akiwa nchini Dubai  mwanamuziki kijana mwenye mafanikio makubwa wa raia wa Marekani Justin Bieber huenda akajikut akihojiwa na Polisi wa nchini humo.

Hiyo ni kufuatia kitendo cha kuendesha gari la kukodi kwa mwendo kasi huku vinasa mwendo vya nchini humo vikishindwa kurekodi mwendo kasi alikuwa nao kwa wakati huo.

Akiwa kwenye gari hilo la kifahari la mwendo kasi kijana huyo alikuwa akiendesha gari hilo kwenye barabara ambayo inaaminika kuwa na vinasa mwendo sita lakini cha hajabu hakuna kilichorekodi mwendo wa gari hilo alilokuwa akiliendesha.
Shuhuda wa tukio hilo Nikki Jameson alisema kuwa Bieber alikuwa akiendesha kwenye mtaa wa Sheikh Zayed Road ambapo karibia kila kamera ilizima muda huo wakati alipopita.

Lakini hata hivyo kun akamera iliyomuonesha akiwa ametokeza kichwa nje karibia nabasi alilopishana nalo wakati akiendesha gazri lake hilo la kifahari.


Justin Bieber alikuwa akiendesha gari hilo la kukodi lenye thamani ya pauni 12,000 kutoka kwenye hoteli ya kifahari ya Burj Al Arab Hotel kuelekea kwenye uwanja wa e Sevens Stadium.

"Huyu yani kwanza bado anahitaji miaka mingine kama miwili hivi ndio aruhusiwe kukodisha gari la aina hiyo katika nchi hii hivyo anaweza kuhojiwa na Polis kuhusiana na sakata hilo zima" alisema shuhuda huyo.


Katika mtiririko mzima wa maonesho ya muziki nchini humo Bieber alichelewa kuanza kwa moja ya onesho lake nchini humo ambapo aliwasiri jukwaani saa mbili baada ya muda wa shoo kuanza na alishidnwa kuomba msamaha kwa hilo.

0 comments: