TOP NEWS

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipiscing elit. Maecenas mattis nisi felis, vel ullamcorper dolor. Integer iaculis nisi id nisl porta vestibulum.

Thursday 20 June 2013

Mwanadada msanii aula dili na Fast Jet








MSANII wa filamu Ndeshi Shoo ametunukiwa kuwa mteja wa laki mbili kutumia huduma ya ndege ya Fast Jet.

Ndeshi  aliwahi kushiriki katika filamu za Lost iliyoigizwa na msanii mahiri Yusuph Mlela na pia ameigiza kwenye filamu ya Fare Game ambayo imeandaliwa na Mzee Chilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere, Ndeshi alisema kuwa kwake imekuwa ni kama bahati kwa kuwa alikuwa na shauku ya kufanya matangazo na kampuni hiyo.

" Hii ni fursa kubwa kwa kuwa nilikuwa nikifikiria kuwa itakuwaje kama msanii pengine kuigiza filamu kwa kupitia kampuni hii"alisema Ndeshi.

Kwa upande wake Meneja Mkuu wa Fast Jet, Tim Lee-Foster alisema kuwa msanii huyo anapatiwa ofa ya siku mbii katika hoteli ya Serena iliyopo kisiwani Zanzibar.

Alisema kuwa msanii huyo amekuwa ni mteja wa laki mbili kukata tiketi ya kusafiria na ndege tangia ilipoanza kutoa huduma ya usafiri hapa nchini.
Mwisho

0 comments: