Ujumbe wa leo kwa wadada wenye kujisahau
Vaa nguo zote upendeze lakini SANDA
ndiyo fasheni ya mwisho, Tembea kote lakini KABURINI ndiyo matembezi ya mwisho.
Panda gari, punda, meli, treni, ndege, ngamia na pikipiki lakini JENEZA ni gari
la mwisho.
Kusanya mali na mizigo mingi ya thamani lakini UDONGO ni mzigo wako
wa mwisho, utapewa majina meengi mazuri ya kukusifia lakin marehemu ndio jina
la mwisho, paka manukato yote mazuri lakin Uvundo ndiyo marashi ya mwisho, lala
kitanda na nyumba nzuri lakin kaburi ndiyo nyumba ya kudumu, linga kwa uzuri na
umbo lako lakin ukifa utabaki mifupa, TUMCHE MWENYEZI MUNGU TUZIKINGE ROHO ZETU
NA MOTO WA JEHANAN!
0 comments: