Jay Z amuibua mdada huyu
BAADA ya kuvivumbua na kuviendeleza vipaji vya
wasanii kama vile Rihanna na Rita Ora msanii mahiri wa Hip Hop Jay-Z kwa sasa
anaingia katika harakati za kumuendeleza msichana mdogo katika tasnia ya
utayarishaji wa muziki.
Kwa sasa Jiga kama anavyofahamika na
watu wengi amemchukua msichana wa miaka 16 raia wa nchini Kanada aitwaye Ebony Oshunrinde aka WONDAGURL kutayarisha iitwayo Magna Carta Holy Grail.
Mwanadada huyo alipata bahati hiyo
ya kuitwa kwenye dili hilo kufuatia rafiki yake ambae pia anafahamiana na Jay
Z.
Kwa sasa ameujnganishwa kwenye dili
hilo ambalo linatarajia kukamilika Almamis ijayo na litashirikisha kampuni ya
simu ya Sumsung.
Dili hilo linampatia fursa mwanadada
huyo kujiingizia fdha nyingi katika
kutayarisha albamu hiyo ambapo pia anaweza kujikuta akijitengenezea
mazingira ya kula feda hizo kirahisi zaidi.
Rafiki huyo wa Jiga itwae Bling king
alisema kuwa amefurahishwa n auwezo wa mwanadasa huyo wa kutayarisha muziki na
kuongeza kuwa anaweza kuwa mtayarishaji bora wa baadae.
Kwa upande wake mwanadada huyo
alisema kuwa kwa upande wake anaona kuwa hiyo ni fursa kubwa kwa kuonesha
ulimwengu kuwa hata wadogo wanaweza kufanya mambo makubwa kwenye muziki.
Pia mwanadada huyo aliwahi
kutengeneza beat kwa kutumia laptop yake na kuituma kwa rafiki wa karibu aitwae
Travis Scott anaefanya kazi kwa ukaribu zaidi na Kanye West pamoja na Jay Z beat hiyo ilikuw ana maadhi ya Raggae.
Mwanadada huyo wa miaka 16 alisema
kuwa alipigiwa simu na rafiki yake huyo akimwambia kuwa anakaribia kuyabadilisha
maisha yake hali ambayo alisema kuwa kwake alikuwa akiona kuwa ni kama ndoto.
“Kwa sasa najua kuwa watu wengi wanataka
kufanya kazi na mimi na huu kwangu naona kuwa ndio mwanzo wa mafanikio kwangu
najisiki furaha sana" alisema mwanadada huyo.
Ebony anaungana na wanadada wengine
kama vile Rihanna na Rita Ora ambao wote waligunduliwa na kuendelezwa vipaji
vyao na Jay Z.
0 comments: